KUFUATIA Mafuriko
yaliyowapata wakazi wa Uzunguzi katika Manispaa ya Tabora na kuwapatia hasara
ya mali na vyakula,Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imetoa msaada wa chakula
kwa waathirika hao wenye thamani ya Shilingi Milioni Moaja na laki mbili.
Akikabidhi msaada huo
Meya wa Manispaa ya Tabora,Gullamhussein Dewji,amesema wameamua kutoa msaada
huo mdogo ili kuwasaidia wananchi hao kwa vile wameathirika kwa vyakula vyao
kuharibiwa na maji.
Mkuu wa wilaya ya
Tabora,Suleiman Kumchaya ametaka msaada huo uwafikie walengwa na watafuatilia
kuhakikisha walengwa kama wamepata msaada huo wa chakula
Kwa upande wao wakazi
wa eneo hilo wameshukuru kwa msaada huo uliotolewa na Halmashauri ya Manispaa
ya Tabora na kwamba utawatosha angalau kwa siku mbili au tatu.
Wakazi wa eneo hilo
walikumbwa na mafuriko wakati wa sikuku za X.mass kufuatia mvua kubwa
iliyonyesha siku ya tarehe Ishirini na Nne,Sikukuu ya Krismas na Tarehe
Ishirini na Saba na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali zao na vyakula.
0 comments:
Post a Comment