BARAZA la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, mkoani
Tabora, limewakataa mwekezaji, Shen na wenzake Wembele Hunting Safaris
wanaofanya kazi za uwindaji katika pori la misitu ya hifadhi iliyoko
wilayani humo.
Tamko hilo limetolewa katika kikao maalumu cha baraza la madiwani wa
halmashauri ya wilaya hiyo kilichoketi juzi katika ukumbi wa Chuo cha
Maendeleo ya Wananchi, FDC, wilayani humo.
Akitoa taarifa ya uamuzi huo kwa niaba ya madiwani, watendaji wa
halmashauri na wananchi, Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Robert Kamoga,
alisema wamechoshwa na vitendo vya unyanyasaji, ubabe, dhuluma, wizi
na uonevu unaofanywa na wawindaji walioko katika mapori ya hifadhi
wilayani humo.
Alisema wawekezaji hao wanajifanya miungu watu na hawajui kama mapori
hayo ni mali ya serikali na msimamizi wake mkuu ni serikali ya wilaya
kupitia baraza la madiwani na watendaji wa halmashauri hiyo.
Alisema mwekezaji Shen kwa kushirikiana na wenzake wamekuwa kero kwa
wananchi wanaoishi karibu na misitu hiyo na anadaiwa kujimilikisha kwa
nguvu hifadhi za misitu ya Tulu, Koga, Kululu na Inyonga East wilayani
humo huku akiuza wanyama na vitalu vya uwindaji kwa wenzake.
“Hawa watu wakati wanaingia walipokewa vizuri na kupewa ushirikiano
na JUHIWAI (Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyama Pori Ipole), lakini sasa
wanataka kujifanya wao ndio serikali, wanauza vitalu vya uwindaji,
wanapiga wananchi ovyo, wanadharau viongozi wa halmashauri akiwemo
Mbunge wa Sikonge, ni lazima waondoke,” alieleza
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment