Home » » SERIKARI YA KIJIJI YATOA MASHARTI KWA WANAOONGELEA

SERIKARI YA KIJIJI YATOA MASHARTI KWA WANAOONGELEA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
SERIKALI ya Kijiji cha Mwanzugi, wilayani Igunga, Tabora imepiga marufuku wananchi kutembea na nguo za ndani baada ya kuogelea katika bwawa la kijiji.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake  juzi, Mtendaji wa Kijiji, Stanly Ngassa, alisena baadhi ya wananchi wamekuwa na tabia  ya kutembea na nguo za ndani mitaani baada ya kuongelea.
Alisema maamuzi hayo yataambatana na hatua kali za kinidhamu kwa wale wote watakaobainika na kuvunja maadili ya Kitanzania na kukiuka maamuzi ya kijiji.
Alisema serikali hiyo inapenda wananchi waogelee na kupumzika katika siku za mapumziko na kuongeza kuwa maadili ya Mtanzania yalindwe kwa hali na mali, ili kukilinda kizazi kijacho dhidi ya mabadiliko ya maadili.
“Tutahakikisha wote watakaobainika kutenda kosa hilo watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo, kwani hatutakubali kuona kitu hiki kinaendelea kutendeka na sisi tuliopewa dhamana tupo, lazima sheria ichukue mkondo wake,” alisema Ngassa.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa