Home » » NHIF KUKOPESHA WATOA HUDUMA BIL.10/-

NHIF KUKOPESHA WATOA HUDUMA BIL.10/-

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), umetenga sh bilioni 10 zitakazokopeshwa kwa watoa huduma, ili kuboresha huduma kwa wanachama wake.
Kaimu Mkurugenzi wa NHIF, Hamis Mdee, alibainisha hayo mjini hapa mwishoni mwa wiki katika taarifa yake kwenye mkutano wa wadau.
Mdee alisema mfuko huo umetenga fedha hizo, ili kuhakikisha wanachama wanapata huduma bora za vipimo.
Alisema fedha hizo zitakopeshwa kwa watoa huduma,  ili kuwawezesha kupata vifaa tiba na kukarabati maeneo ya kutolea huduma.
Aidha, alibainisha utaratibu huo ni wa mikopo nafuu na marejesho yake hayatafanyika kwa fedha taslimu bali kwa kutoa kwenye madai ya watoa huduma yanayowasilishwa kwa ajili ya malipo.
Alisema bodi imeagiza menejimenti kuandaa utaratibu wa kuzizawadia halmashauri zitakazofanya vizuri katika uandikishaji wanachama wa mfuko wa CHF na nyanja nyingine.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa