Home » » WAVUVI HARAMU MWANZUGI WAPIGWA MARUFUKU

WAVUVI HARAMU MWANZUGI WAPIGWA MARUFUKU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WIZARA ya Mifugo na Uvuvi Kanda ya Kati, imewaagiza watu wanaojishughulisha na uvuvi haramu kwenye bwawa la Mwanzugi, wilayani Igunga, mkoani Tabora waache na endapo wataendelea kukaidi amri hiyo hatua zitachukuliwa dhidi yao.
Ofisa uvuvi mfawidhi na uvunaji wa viumbe hai kanda hiyo, Renatus Karumbeta, alisema hayo katika mahojiano maalum na Tanzania Daima baada ya kuwepo kwa malalamiko kwamba licha ya bwawa hilo kufungwa, wapo wavuvi wanaoshirikiana na maofisa uvuvi kuvua nyakati za usiku.
Ofisa huyo mwenye dhamana ya kusimamia ufugaji wa samaki katika mikoa ya Dodoma, Singida na Tabora kuwa idara yake imeanza kupandikiza samaki na mpaka sasa vifaranga 22,000 vya samaki vimepandikishwa katika bwawa la kijiji cha Igogo.
“Kwa hiyo tunashirikiana na serikali ya kijiji na Wilaya ya Igunga kuhakikisha samaki wale wanalindwa ili wawanufaishe wananchi wote,” alisisitiza Karumbeta.
Kwa mujibu wa Karumbeta wadau wao ni halmashauri za wilaya, mji na manispaa zilizopo kwenye mikoa hiyo, alitumia fursa hiyo pia kuzitaka zione umuhimu wa kufugaji samaki kwa kuwa hakuna tatizo la mbegu kama ilivyokuwa awali.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwanzugi, Abeli Nchimo alisema ili kukabiliana na wavuvi haramu, serikali ya kijiji imejipanga kuwatumia askari wa jeshi la jadi ‘sungusungu’ kufanya doria usiku na mchana katika bwawa hilo.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa