Home » » UCHAKAVU WA MAHAKAMA ZA MWANZO WAZUA HOFU

UCHAKAVU WA MAHAKAMA ZA MWANZO WAZUA HOFU

Baadhi ya majengo ya Mahakama za Mwanzo Mkoa wa Tabora yamechakaa na hivyo kuhatarisha usalama wa maisha ya wananchi wanaokwenda kupata huduma kwenye mahakama hizo na hata wafanyakazi wake.
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, Wilfred Dyansobera aliyataja majengo yanayohatarisha maisha ya wananchi na wafanyakazi wake kuwa ni pamoja na yale ya maeneo ya Urambo, Kigwa, Ussoke, Igalula, Sikonge, Ichemba, Isevya na Goweko.
Akizungumza na gazeti hili kuhusu utoaji wa huduma katika Mahakama hizo jana, Naibu msajili huyo alisema, watendaji wa Mahakama hizo wanajitahidi na akiwahimiza wananchi kuhakikisha wanazifahamu haki zao na wakati huohuo kuzisaidia Mahakama kutimiza wajibu wake.
Amewaasa pia watumishi wa Mahakama Kanda ya Tabora, kuzingatia maadili ya kazi zao na akionya mwananchi kupewe huduma baada ya kuinunua na kudai kuwa hilo ni kosa na ni kinyume cha sheria na taratibu zilizowekwa.
Naibu msajili huyo alisema mtumishi wa Mahakama ana wajibu wa kutoa huduma kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo iliyowekwa na kwa muda mwafaka.
Alisema iwapo mtumishi wa mahakama atabainika kutoa huduma kwa kuomba rushwa atakuwa ametenda kosa la jinai na aliyeombwa anaruhusiwa kwenda sehemu nyingine kudai haki itendeke kama Takukuru au Polisi ama kwa mwajiri wake.
Alisema iwapo itathibitika hatua zinaweza kuchukuliwa zikiwamo za kinidhamu kama vile kusimamishwa au kufukuzwa kazi.
Dyansobera alisema iwapo kila upande utafahamu haki na wajibu wake taswira ya Mahakama katika jamii haitachafuka anaamini kuwa Mahakama ni chombo cha kukimbilia kila mtu iwe Serikali au mtu binafsi.
na kwamba lazima iaminiwe na kila mdau anayepewa huduma na chombo hicho.
 ChanzoMwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa