Home » » RAS TABORA AWATAKA MA-DED KUWASHIRIKISHA WAKAGUZI WA NDANI KUHAKIKI UBORA WA MIRADI

RAS TABORA AWATAKA MA-DED KUWASHIRIKISHA WAKAGUZI WA NDANI KUHAKIKI UBORA WA MIRADI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na Tiganya Vincent
RS-Tabora


Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Dkt. Thea Ntara amewataka Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri zote mkoani humo kuwashirikisha Wakaguzi wa Ndani na Maafisa wa Ugavi na Ununuzi wakati wa ukaguzi miradi mbalimbali katika maeneo yao ili kuhakikisha inatekelezwa kwa ubora na inalingana na thamani ya fedha iliyotolewa na Serikali.

Dkt. Ntara ametoa kauli hiyo jana mjini Tabora wakati anafunga mafunzo ya siku tano ya Wakaguzi wa Ndani wa Halmashauri zote ya Mkoa wa Tabora yaliyohusu mbinu mpya za ukaguzi wa hesabu kufuatia mabadiliko katika ukusanyaji wa mapato na maduhuli ya Serikali kuendeshwa kwa njia ya mtandao.

Alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kwa Halmashauri kutopokea miradi iliyotekelezwa chini ya kiwango na hivyo kuiepusha Serikali hasara na kutowakatisha wananchi wanakuwa wanaotarajia mradi uwasaidie.
“Nawagiza Wakurugenzi katika Halmashauri zote nane za Tabora kuhakikisha wanaongozana na Wakaguzi wa Ndani na Maafisa wa manunuzi ili waweze kujiridhisha kama miradi inatekelezwa inalinga na fedha iliyotolewa na hakuna udanganyifu wowote uliofanyika” alisisitiza Dkt. Ntara.

Aidha Dkt. Ntara alitoa kwa Wakaguzi hao wa Ndani waliopata mafunzo hayo na mbinu hizo za kisasa walizofundishwa kufanya kazi kwa ufanisi na kuzisaidia Halmashauri kudhibiti upotevu wa fedha za Serikali katika Halmashauri zao katika makusanyo ya maduhuli na miradi mbalimbali inayotekelezwa katika maeneo yao.

Alisema kuwa mafunzo waliyopata hatakuwa na maana kama hawatasaidia Halmashauri zao katika kudhibiti matumizi mabaya ya maduhuli ya Serikali na hivyo ni vema wakawa wa kwanza kuonyesha udhaifu ili hatimaye yafanyike maboresho.

Mafunzo hayo yaliwashirikishi wa washiriki 15 kutoka Halmashauri zote za Tabora na yalitolewa na Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Idara ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali(IAG) ili kuwajengea uwezo na kuongeza tija katika utendaji wa kazi za kiukaguzi.

Katika mafunzo hayo washiriki walipata mafunzo ya matumizi ya komputya kwa kutumia mbinu za kisasa za ukaguzi kufuatia maduhuli kilipwa kwa njia ya kimtandao.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa