Home » » TAFITI ZA KILIMO ZAWAFIKIA WAKULIMA WA WILAYA YA URAMBO KWA MARA YA KWANZA

TAFITI ZA KILIMO ZAWAFIKIA WAKULIMA WA WILAYA YA URAMBO KWA MARA YA KWANZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Mshauri wa Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange, akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Urambo mkoani Tabora, Angelina Kwinga mbegu ya mihogo inayostahimili ukame katika uzinduzi wa mashamba darasa ya mbegu hiyo ya mihogo, mahindi aina ya Wema 2109  pamoja na viazi lishe yalioanzishwa kwa ajili ya wakulima wa vijiji nane katika wilaya hiyo leo kwa ufadhili wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana  OFAB.



 Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ugalla, Geofrey Magambo akizungumza katika uzinduzi huo wakati akiwatambulisha viongozi mbalimbali wa Kata hiyo na Kijiji cha Isongwa.
 Ofisa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Said Babu akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mshauri wa Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange (kulia), akizungumza kwenye uzinduzi darasa wa shamba la mahindi katika Kijiji cha Isongwa kilichopo Kata ya Ugalla Ussoke wilayani Urambo mkoani Tabora.
 Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora katika uzinduzi wa mashamba darasa hayo ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi, Phillips Mtiba akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo.
 Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora katika uzinduzi wa mashamba darasa hayo ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi, Phillips Mtiba, akikabidhiwa mbegu ya mahindi ya Wema na Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH, Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa.
 Wananchi wa Kijiji cha Isongwa wakisubiri kupata mafunzo ya upandaji wa mbegu ya mahindi katika shamba darasa.
 Mtafiti, Ismail Ngolinda kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga, mkoani Morogoro akitoa maelezo kwa wakulima wa Kijiji cha Isongwa jinsi ya kupanda mahindi aina ya Wema.
 Mkulima wa Kijiji cha Isongwa, Malando Malando akiuliza swali.
 Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Isongwa, Shabani Rajabu Mkokoteni akiuliza swali.
 Wanawake wakulima wa Kijiji cha Isongwa wakijumuika kwenye uzinduzi huo wakiwa na watoto wao.
 Mtafiti, Ismail Ngolinda kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga, mkoani Morogoro, akionesha uchimbaji wa mashimo kabla ya kupanda mbegu hiyo ya mahindi.
 Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Isongwa, Shabani Rajabu Mkokoteni , akichimba mashimo.
 Mtafiti, Ismail Ngolinda kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga, mkoani Morogoro, akionesha, akionesha namna ya kuweka mbolea kwenye mashimo yaliyochimbwa.
  Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora katika uzinduzi wa mashamba darasa hayo ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi, Phillips Mtiba, akipanda mahindi.
 Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH, Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa, akipanda mahindi.



 Mwenyekiti wa Halmshauri ya wilaya hiyo Adamu Malunkwi, akizungumza na wakulima wakati wa uzinduzi huo.
 Mtafiti wa Mazao ya Mizizi kutoka Kituo cha Ufatiti cha Maruku mkoani Kagera, Jojianas Kibura, akiwaelekeza wakulima wa Kijiji cha Usisya namna ya kupanda mbegu ya viazi lishe.
 Wakulima wa Kijiji cha Kapiluka wakijiandaa kupanda mbegu ya viazi lishe.
Mtafiti wa Mazao ya Mizizi kutoka Kituo cha Ufatiti cha Maruku mkoani Kagera, Jojianas Kibura, akiwaelekeza wakulima wa Kijiji cha Motomoto namna ya kupanda mbegu ya viazi lishe.

Na Dotto Mwaibale, Urambo Tabora

TAFITI za kilimo zinazofanywa hapa nchini na wataalamu zimewafikia wakulima wa Wilaya ya Urambo mkoani Tabora kwa mara ya kwanza.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Halmshauri ya wilaya hiyo Adamu Malunkwi wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye uzinduzi na kukabidhi mbegu bora za Mahindi ya Wema 2109 na mihogo kwa ajili ya mashamba darasa kwa wakulima wa vijiji nane vya Isongwa, Ussoke, Usisya, Kapiluka, Vumilia, Kamalendi, Muungano na Songambele.

Alisema mara nyingi tafiti zilizokuwa zikifanyika zilikuwa zikibaki kwenye makabati bila ya kuwafikia walengwa na jambo lililofanywa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB) kuwafikishia wakulima matokeo ya tafiti hizo ni jambo zuri na limefurahiwa na kwa hapa kwetu ni mara ya kwanza kutokea.

"Tuna amini kuwa hivi sasa uchumi utastawi kuanzia ngazi ya familia, wilaya na hadi taifa na tutakuwa na chakula cha kutosha" alisema Malunkwi.

Malunkwi alisema katika wilaya hiyo walikuwa na changamoto kubwa ya kupata mbegu bora kwani wakulima wengi walikuwa wakitumia mbegu za zamani walizozizoea na kujikuta wakipata mazao kiduchu lakini kwa ujio wa mbegu hizo ni ukombozi mkubwa kwao.

Alitaja changamoto nyingine ambayo inapaswa kuangaliwa kwa karibu kuwa ni bei kubwa ya mbegu hiyo ya mahindi ambayo inauzwa shilingi 12,000 kwa kilo mbili huku kukiwa na debe moja la mahindi linalouzwa shilingi 10,000 ambalo wakulima wamekuwa wakilikimbilia kutokana na bei yake kuwa ya chini ingawa mazao yake hayana tija.

Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa, alisema mbegu hiyo ya mahindi imefanyiwa utafiti na inavumilia ukame wakati ile ya mihogo ikivumilia magonjwa kama batobato na michirizi kahawia huku zikitoa mavuno mengi.

Alisema COSTECH katika mkoa huo imetoa kilo 60 za mbegu ya Wema, mihogo 40,000 na viazi lishe 75 ambapo katika wilaya hiyo vijiji nane vimenufaika kwa ajili ya kutengeneza mashamba darasa ambayo yatatoa mbegu zitakazosambazwa kwa wakulima katika maeneo mengine. 

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora katika uzinduzi wa mashamba darasa hayo ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi, Phillips Mtiba alisema hivi sasa mwajiriwa ni mkulima ambaye analima kilimo chenye tija na si vinginevyo na kuwa serikali siku zote imekuwa ikihimiza kilimo bora ambapo aliwataka maofisa ugani kupanga ratiba za kuwafikia wakulima.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Angelina Kwinga aliishukuru COSTECH na OFAB kwa kutekeleza ahadi ya kuwapelekea mbegu kama walivyo ahidi walipokuwa wakitoa mafunzo kwa maofisa ugani wa wilaya hiyo mapema mwaka huu.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712727062)

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa